Yacouba Songne jana alicheza kwa takribani dakika 15 kwenye mchezo wa kombe la Mapinduzi dhidi ya KMKM
Kuingia kwake pamoja na kiungo Mudathir Yahya waliongeza kasi ya mashambulizi na hatimaye Yanga kufunga bao dakika ya 95 kupitia kwa Dickson Ambundo
Dakika 15 zilitosha kuwakumbusha Wananchi yule Yacouba wa mwanzoni mwa msimu uliopita
Yacouba huenda akapata dakika nyingi zaidi za kucheza kwenye mchezo unaofuata dhidi ya Singida BS
Yacouba na Lazarus Kambole wamepewa nafasi katika michuano ya kombe la Mapinduzi benchi la ufundi likiwafanyia tathmini kuona utayari wao baada ya kuwa nje kwa muda mrefu wakiwa ni majeruhi