Kiungo fundi Khalid Aucho maarufu 'Dokta' ameongeza mkataba wa miaka miwili kuendelea kuitumikia Yanga
Hivi karibuni ziliibuka tetesi kuwa Aucho anaondoka, Rais wa Yanga Injinia Hersi Said amezima tetesi hizo
Uongozi wa Yanga unaendelea kuhuisha mikataba ya wachezaji wake ambao mikataba yao inaelekea ukingoni
Yanga imejipanga na inahakikisha hakuna mchezaji muhimu anaondoka