Yanga imekamilisha usajili wa kiungo Mudathir Yahya
Mudathir anatua Yanga akiwa mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba na Azam Fc
Baada ya kusaini mkataba mchana wa leo Mudathir ameelekea Zanzibar kuungana na wenzake.
Mudathir anatua kuongeza nguvu katika eneo la kiungo la Yanga hasa wakati huu ambao Yanga wako kwenye mgogoro na Feisal Salum
Mudathir anamudu vyema kucheza nafasi zote za kiungo