YANGA Princess imetuma ujumbe mzito kwa timu zinazoshiriki Ligi ya Wanawake msimu huu baada ya kuichapa bila huruma Mkwawa Queens kwa mabao 4-0.
HAYA HAPA MATOKEO YA SIMBA QUEEN LEO DHIDI YA THE TIGER
Mabao ya Princess kwenye mchezo huu yalifungwa na Wogu Chioma, Anela, Nkor Blessing na Precious Onyinyechi ukiwa na mpira wake wa kwanza kuugusa baada ya kuingia uwanjani.
Ushindi huu umeiongezea Yanga Princess kujiamini kuelekea ‘Derby’ dhidi ya Simba Queens, mchezo utakaopigwa Desemba 22, 2022.